Posts

Mambo haya 10 yatakusaidia kuishi kwa amani.

  Wakuu habari za wakati, nina imani tu wazima wa afya ila kwa wagonjwa Mungu awape tumaini. Leo  Number ni 26  nimeona ni share nanyi kitu kidogo. Yafuatayo yatakusaidia wewe na mimi walau kidogo tukapunguza kuwa na "makasiriko" kati yetu na kufanya amani itawale:- 1. MUNGU. Kuna msemo unasema "God first", yes nadhani katika harakati zetu tukimuweka mbele Yeye basi kifuatacho ni AMANI 2. SAMEHE. Hii ni moja ya sababu inayowafanya wengi wapate "jaka la moyo" ni kushindwa kusamehe. Hebu samehe sasa upate AMANI na afya 3. ISHI MAISHA YAKO. Yes hebu fanya kama una deal na mambo yako uone kama hutopata AMANI. Acha kufatilia ya watu utakufa 4. ONDOA MAWAZO HASI. Hebu acha hiyo dhana ya mtu akifanya kitu/jambo basi wewe ni kukosoa tu, hivi utapata AMANI kwa style hiyo? Mwisho utakuwa mchawi sasa 5. KUWA NA SHUKURANI. Vitu vidogo tu vinaweza kukupotezea AMANI moyoni, kumbe ukishukuru kwa vitu kama afya, pumzi, mazingira, kuamka salama, kupenda & kupendwa nk.....

Haya mambo 30 yanayonisumbua sana, sijui wewe

  Katika mambo yanayonisumbua maisha yangu, mambo haya 30 yanaongoza; 1. Kila kitu ni kitapita au ni cha muda tu ukiwemo uhai au maisha yangu. 2. Ukweli kuwa sitoridhika na nilichonacho au niliyonayo mpaka wakati wa kufa 3. Uhalisia kuwa uchu ndiyo unaotawala uchumi na uchumi nao kutawala uchu. 4. Kuwa na marafiki wengi siyo uhakika wa furaha 5. Ukweli kuwa marafiki wa karibu ndiyo watakaonikimbia wakati wa changamoto 6. Pesa siyo kila kitu ila kila kitu kinahitaji pesa. 7. Kila mtu ni mbinafsi ila huifanya kazi isiyo na tija ya kuuficha. 8. Ulimwengu unavyofundisha mtu kujithamini kwanza kabla ya kuwataka wengine wamthamini. 9. Hakuna ajuaye yatakayotokea au kesho (wakati ujao) 10. Kamwe huwezi kuelewa mafanikio kama hujaionja ladha ya kutofanikiwa. 11. Unatafsirika kwa kile unachojua na siyo kile unachomiliki. 12. Kufanya ni vizuri kuliko kufikiri. 13. Kusamehe ni sawa kuupanda mlima mkubwa. 14. Maisha unayoyataka kuyaishi yanatafsiriwa na wewe. 15.Baadhi ya watu siyo wa kiwango ...

Ukiwa na haya umekula bingo Kwa Zama hizi

  Salama! Siku hizi nimekua mkubwa, mambo ya kuandika madude marefu nimewaachia wengine. Haya nisipoteze muda. Siku hizi ukiwa na mambo haya basi jua umeula, umelamba dume, umekula bingo. Ni wewe tuu kuamua utoboe au usitoboe. 1. Kujua kingereza au lugha yoyote kubwa kimataifa. Achaneni na kile kingereza cha kulambia chumvi nazungumzia ujue kingereza kabisa au lugha kama kichina, kiarabu, kireno au kihispania. Umeula, yaani ushindwe mwenyewe. Huwezi ukajua kingereza au lugha za kimataifa alafu Maisha yakakushinda. Tena ukiwa Jiji kama Dar na Arusha. Sio ujue kingereza alafu ukajichimbie Huko mkoani. Utakwama. Ukijua Lugha ya kingereza, itakupasa uwe na Smartphone au Laptop, itakupasa uwe na Akili ya kuchangamana na watu. Keisha!! 2. Kipaji Ukijua kuimba, mchekeshaji, kuchora, kusuka, Kwa kiwango cha juu. Maisha yakikushinda umeamua mwenyewe. Tatizo la Vijana wengi wa Kitanzania wanasubiri mpaka wawezeshwe. Utahitaji tuu smartphone na bando lako. Jitangaze, kuliko ukae hivihivi ni b...

Ukitumia hii dawa yenye mchanganyiko wa mizizi sita, utavuta wateja kwenye biashara yako mpaka watu washangae

  Kifungua kinywa cha asubuhi ni chai lakini kifungua kinywa cha waungwana ni salamu. Salamu kwenu wanafamilia wa JamiiForums, ni imani yangu kuwa mu wazima wa afya na poleni sana mashabiki wa Simba damudamu, kwa shambulizi la risasi moja ya kichwa, mliyofyatuliwa na Wanajeshi wa Yanga kwenye vita ya kombe la Ngao ya Jamii pale Uwanja wa Benjamini Mkapa. Ningekuwa mchoyo wa nidhamu na msaliti wa mila na desturi za Kiafrika, endapo ningeanza kuandika makala hii bila kuwasalimu. "Nasikitika kuwa, hii video niliyosema uitazame, ipo kwenye simu lakini kila nikitaka kuambatanisha video (attach file) inashindikana na haiwezekani kuhariri kichwa cha habari kikishaenda hewani, mtanisamehe". Baada ya kutimiza jukumu hilo la kinidhamu, niende moja kwa moja kueleza na kufafanua makala yetu tajwa. Ujasiriamali umekuwa ni chanzo kikubwa cha ajira kwa Watanzania wengi. Wanawake kwa wanaume, vijana kwa wazee, wamekuwa wakijihusisha na biashara ndogondogo ili kuweza kujikimu na maisha. Akina...

Nataka Kubadilika: Mambo 10 muhimu unayotakiwa kuyaacha

Image
  MAMBO 10 MUHIMU UNAYOTAKIWA KUYAACHA. Rafiki yangu mpendwa, Unashindwa kutoka hapo ulipo siyo kwa sababu hutaki kutoka hapo ulipo, hapana, unataka sana tu kutoka hapo ulipo na kufika kule unapotaka wewe kufika. Ila tatizo lako wewe ni kuwa unataka kutoka hapo ulipo kwa maneno na si kwa vitendo yaani bado hujadhamiria kweli kutoka hapo ulipo. Ziache tabia hizi kumi mara moja ili uweze kutoka hapo ulipo na kusonga mbele. Moja Tabia Ya Kujilinganisha Na Wengine. Theodore Roosevelt aliwahi kusema kwamba, "Comparison is the thief of joy." Akiwa na maana kwamba, "Tabia ya kujilinganisha na wengine ni mwizi wa furaha yako." Kama ungelijua kuwa miongoni mwa sumu mbaya na hatari kwa Mafanikio yako basi hii tabia ya kujilinganisha na wengine ni hatari sana. Iache mara moja, Mtu pekee wa kujilinganisha nae ni wewe mwenyewe. Ukijilinganisha na watu kwa hakika utaishia kufadhaika kwani kunafadhaisha sana. Mbili Tabia Ya Kusubiria Mpaka Uwe Tayari. Ukisubiri mpaka uwe tayari nd...